Ticker

6/recent/ticker-posts

Wahitimu UDSM Wahimizwa Kutafuta Fursa Mbadala za Ajira

MAKAMU Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. William Anangisye, amewahimiza wahitimu wa chuo hicho kutokaa wanasubiri ajira za serikalini pekee, bali pia kuangalia fursa nyingine za kiuchumi kwa kutumia maarifa na ujuzi waliyojifunza.

Akizungumza katika Mahafali ya 54 ya chuo hicho, Prof. Anangisye alisema elimu inawainua wahitimu na kuongeza thamani yao katika jamii, hivyo ni muhimu kutumia maarifa hayo kutatua changamoto zinazowakabili Watanzania.

Aliwakumbusha wahitimu umuhimu wa kuwa wabunifu na kuchangia katika maendeleo ya taifa, akirejea kauli ya Mwalimu Julius Nyerere kuhusu matumizi ya rasilimali katika kuwekeza katika elimu.

Alisisitiza kuwa wazazi na wadau wanapaswa kuunga mkono juhudi za serikali katika kuwekeza katika elimu.

Prof. Anangisye alitoa wito kwa wahitimu kurejea ofisini kwa kuzingatia sheria na maadili ya utumishi wa umma, akisisitiza umuhimu wa kuwa na uadilifu katika kazi zao.

Alimshukuru Mkuu wa Chuo, Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete, pamoja na Baraza la Chuo na wadau kwa mchango wao katika mafanikio ya mahafali haya.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Chuo, Balozi Mwanaidi Maajar, aliwasihi wahitimu kuwa na busara na kuongeza bidii katika kutafuta fursa halali za kujiendeleza, huku akisisitiza umuhimu wa kujifunza kutoka kwa changamoto za maisha.

Post a Comment

0 Comments