Ticker

6/recent/ticker-posts

Mahafali ya 16 ya Bethsaida: Wahitimu Wasisitizwa Thamani ya Elimu na Uadilifu

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

WAHITIMU wa kidato cha nne Shule ya Sekondari Bethsaida wametakiwa kuendelea kuwa waadilifu na kuwa mfano mzuri katika jamii, huku wakisisitiza kuwa ni jukumu lao kuimarisha maadili na ujuzi waliyopata shuleni.

Wito huo umetolewa leo Oktoba 19, 2024 katika Mahafali 16 ya shule hiyo iliyopo Mbezi Mpiji Magoe Jijini Dar es Salaam na Constantine Kaniki ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye hafla hiyo.

Amesema kuwa kutokana na changamoto ya ajira nchini, wanafunzi wanatakiwa kufahamu na kujiandaa kutafuta fursa za kujiajiri badala ya kutegemea kuajiriwa pindi watakapomaliza masomo yao.

Aidha amesisitiza umuhimu wa elimu kama daraja kuelekea mafanikio, huku akiwasisitizia wahitimu kuwa mafanikio hayaji kirahisi na yanahitaji juhudi na ubunifu.

Pamoja na hayo amewapongeza viongozi wa shule hiyo kwa  kukaa na kuamua kuokoa maisha ya watoto , hasa  hawa wa jinsia ya kike ambao mara nyingi ndio wanaoangukia kwenye kundi la waathirika wa matukio.

"Ni watoto wengi sana wanaachwa wakitaabika mitaani bila msaada, na kwa hatua hii mliyochukua ya kuanzisha hiki kituo na shule, na kwa hatua mliyofikia  ikiwemo mafanikio ya kielimu kwa wanafunzi wanaopitia shule tokea ilipoanzishwa. Hivyo mnapaswa kupewa pongezi kubwa sana". Amesema

Amewapongeza taasisi za dini, wahisani na wafadhili, pamoja wadau mbalimbali ambao wamekuwa wakitoa michango yao ambayo inaiwezesha shule hiyo  kutekeleza majukumu yake katika nyanja za ufundishaji  na kutoa huduma ya kuyanusuru  maisha  ya watoto hao.

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Holliness Mushi amesema lengo la kuanzishwa kwa shule hiyo lilikuwa ni kuipunguzia serikali mzigo mkubwa wa watoto yatima au wale wanaoishi katika mazingira magumu kwa lengo la kuwapatia elimu bora kama ilivyo kwa watoto wengine.

"Lengo la kuanzisha shule hii pia ni kupunguza uwezekano wa kufanyiwa vitendo vya ukatili majumbani na mitaani watoto wa namna hii; mfano ubakaji, kunyimwa haki zao za msingi ambapo hapa tunawaanda kuwa watu bora, wazalishaji na wenye thamani katika jamii na pia wenye kujiamini". Amesema

Amesema ufaulu wa wanafunzi umezidi kukua kwani mwaka jana asilimia 90 yaani 26/29 walijiunga na masomo ya kidato cha tano na wengine walijiunga na vyuo vya kati. Hakukuwa na mwanafunzi aliyefeli kwa kupata zero. 

Amesema kwa mwaka huu 2024, wanafunzi wote walipata division I, II, na III tu, hakukuwa na Four wala zero katika mtihani wa mock wa kidato cha nne.

" Tunajivunia matokeo ya watoto wetu kwani yanatokana na juhudi zao pamoja na kazi nzuri inayofanywa na timu ya waalimu wetu. Karibu kila mwaka angalau asilimia tisini (90%) ya wanafunzi wote wanaomaliza kidato cha nne  huchaguliwa kuendelea na masomo ya kidato cha tano ama vyuoni. Ameeleza.

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya Shule ya Sekondari ya  Bethsaida, Raymond Machary amewatia moyo wahitimu hao kwa kuwaambia wanapoelekea katika mitihani yao ya mwisho wasiwe na woga bali wajiandae vizuri  ili kesho yao waweze kuwasaidia wazazi.

Aidha Machary amewaomba wazazi kuwa sehemu ya faraja kwa watoto hao na kuwasaidia katika nyanja zote ikiwemo ya  kiuchumi kwani kufanya hivyo watasaidia  kukidhi mahitaji yao.

"Tunaamini mnaweza lakini chochote ambacho mtakuwa mmebarikiwa na mwenyezi Mungu mkitoa katika fungu la kumi mtabarikiwa na Mwenyezi Mungu"Amesema.
 
Shule ya Sekondari Bethsaida ambayo ni ya wasichana hususan wale ambao ni yatima na ambao wazazi wao hawajiwezi ilianza kama kituo cha kulelea watoto yatima mwaka 2005 na hatimaye kuwa shule ya upili mwaka 2006, ambapo mpaka sasa ni Mahafali ya 16 na kwa mwaka huu 2024 wahitimu 35 wameza kuhitimu masomo ya kidato cha nne.
Constantine Kaniki ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye Mahafali ya 16 ya kidato cha nne shule ya sekondari Bethsaida akikabidhi vyeti kwa wahitimu leo Oktoba 19, 2024 katika viwanja vya shule hiyo Jijini Dar es Salaam
Constantine Kaniki ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye Mahafali ya 16 ya kidato cha nne shule ya sekondari Bethsaida akikabidhi vyeti kwa wahitimu leo Oktoba 19, 2024 katika viwanja vya shule hiyo Jijini Dar es Salaam
Constantine Kaniki ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye Mahafali ya 16 ya kidato cha nne shule ya sekondari Bethsaida akikabidhi vyeti kwa wahitimu leo Oktoba 19, 2024 katika viwanja vya shule hiyo Jijini Dar es Salaam
Constantine Kaniki ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye Mahafali ya 16 ya kidato cha nne shule ya sekondari Bethsaida akikabidhi vyeti kwa wahitimu leo Oktoba 19, 2024 katika viwanja vya shule hiyo Jijini Dar es Salaam
Constantine Kaniki ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye Mahafali ya 16 ya kidato cha nne shule ya sekondari Bethsaida akikabidhi vyeti kwa wahitimu leo Oktoba 19, 2024 katika viwanja vya shule hiyo Jijini Dar es Salaam
Wazazi na walezi wakiangalia bunifu zilizofanywa na wanafunzi wa shule ya sekondari Bethsaida wakati wa Mahafali ya 16 ya kidato cha nne shule hiyo yaliyofanyika leo Oktoba 19, 2024 Jijini Dar es Salaam.
Wazazi na walezi wakiangalia bunifu zilizofanywa na wanafunzi wa shule ya sekondari Bethsaida wakati wa Mahafali ya 16 ya kidato cha nne shule hiyo yaliyofanyika leo Oktoba 19, 2024 Jijini Dar es Salaam.
Wazazi na walezi wakiangalia bunifu zilizofanywa na wanafunzi wa shule ya sekondari Bethsaida wakati wa Mahafali ya 16 ya kidato cha nne shule hiyo yaliyofanyika leo Oktoba 19, 2024 Jijini Dar es Salaam.
Wazazi na walezi wakiangalia bunifu zilizofanywa na wanafunzi wa shule ya sekondari Bethsaida wakati wa Mahafali ya 16 ya kidato cha nne shule hiyo yaliyofanyika leo Oktoba 19, 2024 Jijini Dar es Salaam.
Wahitimu wa kidato cha nne shule ya sekondari Bethsaida wakitoa burudani wakati wa Mahafali ya 16 ya kidato cha nne shule hiyo yaliyofanyika leo Oktoba 19, 2024 Jijini Dar es Salaam.
Constantine Kaniki ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye Mahafali ya 16 ya kidato cha nne shule ya sekondari Bethsaida akizungumza kwenye mahafali hayo ambayo yamefanyika leo Oktoba 19, 2024 Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya Shule ya Sekondari ya  Bethsaida, Raymond Machary akizungumza kwenye Mahafali ya 16 ya kidato cha nne ya shule hiyo ambayo yamefanyika leo Oktoba 19, 2024 Jijini Dar es Salaam.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Bethsaida, Holliness Mushi akizungumza kwenye Mahafali ya 16 ya kidato cha nne ya shule hiyo ambayo yamefanyika leo Oktoba 19, 2024 Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wazazi na walezi wa wanafunzi wakiwa katika Mahafali ya 16 ya kidato cha nne ya shule ya Sekondari ya Bethsaida ambayo yamefanyika leo Oktoba 19, 2024 Jijini Dar es Salaam.
Constantine Kaniki ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye Mahafali ya 16 ya kidato cha nne shule ya sekondari Bethsaida akiwa pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya Shule ya Sekondari ya  Bethsaida, Raymond Machary wakipata picha ya pamoja na wahitimu 35 wa kidato cha nne wa shule hiyo katika Mahafali ya 16 ya kidato cha nne ambayo yamefanyika  leo Oktoba 19, 2024 Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

Post a Comment

0 Comments