Ticker

6/recent/ticker-posts

HAMUOGOPI? CCM ‘WATISHA’, NCHIMBI AKIZUNGUMZA NAO KAHAMA

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akizungumza kwenye mkutano wa ndani wa wanachama na viongozi wa CCM Wilaya ya Kahama, tarehe 10 Oktoba 2024, baada ya kupokelewa rasmi wilayani humo leo asubuhi, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kikazi Mkoa wa Shinyanga, ambayo leo imeingia siku ya pili. 

Balozi Nchimbi, ambaye ameambatana na Katibu wa NEC - Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Ndugu Amos Gabriel Makalla na Katibu wa NEC - Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Ndugu Rabia Hamid Abdalla, baadae jioni anatarajiwa kuzungumza na wananchi wa Kahama katika mkutano mkubwa wa hadhara, Uwanja wa Stendi Ndogo ya Malori, mjini Kahama.

Post a Comment

0 Comments