Ticker

6/recent/ticker-posts

DC KARATU AIPONGEZA CARMATEC KWA KUSAMBAZA MASHINE KWA WAKULIMA KARATU.


Ferdinand Shayo ,Arusha.

Mkuu wa Wilaya ya Karatu Dadi Kolimba amekipongeza Kituo cha Zana za Kilimo na Teknolojia vijijini (CAMARTEC) kwa kusambaza teknolojia na mashine mbali mbali za kulima ,kuvuna na kuchakata mazao pamoja na kuyaongezea thamani ili yaweze kupata bei nzuri katika masoko ya ndani na nje ya nchi hivyo kuwakomboa wakulima.

Akizungumza mara baada ya kutembelea kituo kihandisi cha Teknolojia za Kilimo kilichoanzishwa na CAMARTEC katika kijiji cha Gongali Wilayani Karatu ambapo amejionea zana mbali mbali ikiwemo mashine za Kupukuchua mahindi,maharage,alizeti na matrekta ,Mkuu wa Wilaya hiyo amesema kuwa kituo hicho kitawasaidia wakulima kulima kwa kisasa na kuchakata mazao yao kwa kutumia zana za kisasa.

Kolimba ameipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kuiwezesha Camartec kufungua kituo kijijini hapo na kuwafikia wakulima wengi na kuongeza kuwa uhitaji wa mashine hizo bado ni mkubwa kwa wilaya hiyo yenye wakulima wengi zaidi.

Kaimu Mkurugenzi wa CARMATEC Mhandisi Godfrey Mwinama amesema wataendelea kufanya utafiti na kutengeneza mashine ambazo zitakua mkombozi kwa wakulima kwa kuwokolea muda na gharama lunwa walizokuwa wakitumia kutokana na teknolojia duni.

"Tunaishukuru sana Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dr
Samia Suluhu Hassan kwa kutuwezesha kuwasogezea wakulima wa vijijini mashine mbali mbali " Anaeleza Godfrey Mwinama Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa CARMATEC. 

Kwa upande wao wakulima wakiwemo Rogati Israel na Musa Hussein wamesema kuwa mashine walizozipata kutoka CAMARTEC Zimewasaidia kupukuchua mahindi na maharage kwa muda mfupi bila kuharibu ubora wa mazao hayo.

Post a Comment

0 Comments