Ticker

6/recent/ticker-posts

LALJI FOUNDATION YAKABIDHI MADAWATI 100 KWA SHULE 2 ZA WILAYA YA KISARAWE


Taasisi isiyo ya kiserikali ya LALJI FOUNDATION imetoa msaada wa madawati 100 kwa shule za msingi 2 Wilayani Kisarawe ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za serikali kuboresha mazingira ya sekta ya elimu nchini.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi madawati hayo kwa shule za msingi Msanga na Bembeza makamu Mwenyekiti taasisi ya LALJI FOUNDATION Mohamed Damji amesema kuwa wametoa madawati hayo kwaajili ya kuunga mkono juhudi za serikali ya Tanzania kuboresha miundombinu na mazingira ya elimu nchini.

Aidha Bw. Damji amewataka wanafunzi wa shule hizo kusoma kwa bidii ili kufikia malengo yao ikiwemo kuwa viongozi bora na kufanya kazi katika fani mbalimbali hapa nchini.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe Mh. Zuberi Kizwezwe ameishukuru taasisi ya LALJI FOUNDATION kwa kutoa msaada huo na kutoa wito kwa taasisi nyingine kuiga mfano kutoka taasisi hiyo kutoa misaada mbalimbali katika6 jamii.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Mh. Petro Magoti amesema Wilaya ya Kisarawe itaendelea kushirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali na wadau wa maendeleo katika mambo mbalimbali huku akishukuru na kuipongeza taasisi ya LALJI FOUNDATION kwa kuendelea kusaidia jamii ya watu wenye uhitaji.

Post a Comment

0 Comments