Ticker

6/recent/ticker-posts

JESHI LA ZIMAMOTO TANGA WAJA NA PROGRAMU ZA KUELIMISHA UMMA NAMNA KUKABILIANA NA MAJANGA YA MOTO


Na Oscar Assenga,TANGA

JESHI la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Tanga wameanzisha program mbalimbali za kuielimisha Umma kuweza kuwa na utambuzi ili majanga ya moto yanapotokea waweze kukabiliana nayo.

Hayo yalibainishwa leo na Afisa Operesheni wa Jeshi hilo mkoani Tanga Mrakibu Msaidizi wa Jeshi hilo Yusuf Msuya wakati akizungumza na kuhusu namna walivyojipanga kukabiliana na matukio ya moto kwa wananchi.

Alisema katika kuzuia ajali za moto wameamua kuja na mpango huo ambao wanaamini utakuwa na mafanikio makubwa ambao utakwenda sambamba na

ukaguzi wa kinga na tahadhari kwa majanga katika maeneo mablimbali yakiwemo ya biashara,makazi na vyombo bya usafiri na usafirishaji.

“Lengo la ukaguzi huu ni kutambua yale mapungufu na risk zilizopo kwenye majengo ambayo ni hatari na kuyawasilisha kwa mmiliki ikiwemo kumpa mapendekezo na hatua za kufanya ili kuzuia moto usitokee “Alisema

Msuya alisema na endapo moto unapotokea madhara yake yawe machache kwa maisha ya wakazi wa Jengo au wafanyakazi wa eneo husika na ambaye atakidhi vigezo vya kukabuliana na majanga ya moto watatoa cheti kutoka Jeshi hilo cha kuonyesha eneo limekaguliwa na kukidhi vigezo vya usalama wa moto .

,”Katika kulipambanua hili nitoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Tanga kufika kwenye ofisi zetu zilizopo maeneo mbalimbali kwa ajili ya kupatiwa wataalamu kwa lengo la kwenda kukagua vyombo vyao vya usafiri iwe nchi kavu au majini pamoja na maeneo ya Biashara na ya makazi uli kuimarisha usalama dhidi ya majanga ya moto kwenye maeneo yao”Alisema

Awali akizungumzia mpango huo Mfanyabiashara katika soko la Mgandini Jijini Tanga Rashidi Said Kihondo alisema kwamba iwapo wataanzisha mpango huo utawasaidia kuweza kukabiliana na moto hivyo kupunguza majanga hayo katika maeneo yao.

“Huko nyuma tuliwahi kukutana na janga la moto na soko liliungua kutokana lakini kwa sasa kutokana na baadhi ya elimu ya kukabiliana na majanga hayo ya moto tulianza kuchukua tahadhari na hayajaweza kujitokeza tena”Alisema

Naye wa upande wake Mfanyabiashara wa soko Makorora Jijini Tanga Mwanahamisi Bakari alisema kwamba elimu hiyo iwapo elimu hiyo itatolewa kwa wafanyabiashara itawawezesha kukabiliana na majanga ya moto na kuweza kuyadhibiti pindi yanapojitokeza na hivyo kutokuwa na adhari kubwa kwao.

Post a Comment

0 Comments