Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS SAMIA AKAGUA MABANDA MBALIMBALI KWENYE MAONESHO YA KIMATAIFA YA WAKULIMA NANE NANE JIJINI MBEYA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) Dkt. Amos Nungu kuhusu Tume hiyo inavyowasaidia wakulima wenye ubunifu mbalimbali katika Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane yaliyofanyika kwenye viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisikiliza maelezo ya mnufaika wa Mpango wa kuwawezesha Vijana kwenye Mifugo (BBT life Mifugo) Rest Mgonja kuhusiana na Mafanikio waliyopata kutokana na mradi huo wa ufugaji wa ng’ombe wa kisasa wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mkurugenzi wa Kampuni ya Asas Bw. Ahmed Salim kuhusu ufugaji wa kisasa wa kondoo na mbuzi wa maziwa wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo wakati alipotembelea vizimba vya kufugia Samaki katika moja ya mabanda ya Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera wakati akiangalia video fupi ya masuala ya Kilimo wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapa chakula Samaki wanaofugwa kwenye vizimba wakati alipotembelea mabanda mbalimbali ya Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Watoto wakati alipokuwa akipita kwenye mabanda mbalimbali ya Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Gerald Mweli pamoja na Dkt. Hussein Mohammed Omar Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo wakati akikata utepe kuashiria uzinduzi wa ugawaji wa vifaa vya maafisa ugani, trekta kwa wakulima, vifaa vya kutengeneza Vihenge vya chuma kwa Vijana, bei elekezi za mbolea ya ruzuku, mradi wa uchimbaji wa visima pamoja na ugawaji wa vifaa vya mfumo wa umwagiliaji kwa matone katika Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane yaliyofanyika Kitaifa Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika viwanja vya John Mwakangale kwa ajili ya kushiriki kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane Kitaifa Mkoani Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.

Mazao mbalimbali ya Kilimo pamoja na mbogamboga zikiwa zimefungashwa vizuri katika Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane yaliyofanyika Kitaifa kwenye viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mkurugenzi wa AVOAFRICA Tanzania Ltd Nagib Karmali kuhusu namna alivyoitikia wito wa Rais Samia kuja Tanzania kuwekeza kwenye Kilimo cha Parachichi katika Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane yaliyofanyika kwenye viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe kuhusiana na mbegu bora za zao la Alizeti katika Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane yaliyofanyika kwenye viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasikiliza Vijana waliohitimu Mafunzo ya Elimu ya Juu na kujiingiza kwenye masuala ya Kilimo na kuelezea jinsi walivyofanikiwa kwenye Sekta hiyo katika viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) Dkt. Amos Nungu kuhusu namna ya kuwapa chanjo Samaki wakiwa ndani ya maji katika Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane kwenye viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mhandisi wa Mtaani (Street Engineer) Adam Zacharia Kinyekile kutoka Tunduma Mkoani Songwe jinsi alivyobuni na kutengeneza mashine hiyo ya kuvuta maji, kupukuchua mahindi kusaga nafaka pamoja na kubeba Mizigo wakati wa Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane ambapo Kitaifa yamefanyika katika viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mwanzilishi wa Kampuni ya Avomeru Bw. Jesse Oljange kuhusu ukamuaji wa mafuta mbalimbali ikiwemo ya zao la parachichi katika Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nane Nane yaliyofanyika Kitaifa kwenye viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya tarehe 8 Agosti, 2023.

Post a Comment

0 Comments