Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS DKT. MWINYI AJUMUIKA NA WANANCHI KATIKA DUA NA SALA YA MAITI YA MAREHEMU HASSAN MOHAMMED SAID ILIYOFANYIKA KATIKA MASJID JAMIU ZINJIBAR MAZIZINI

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Waumini katika kupokea jeneza likiwa na mwili marehemu Hassan Mohammed Said, katika Masjid Jamiu Zinjibar Mazizini Unguja kwa ajili ya Ibada ya Sala ya Maiti iliyofanyika katika Masjid hiyo leo 31-8-2023,na (kushoto kwa Rais) Ndugu wa marehemu Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mhe. Simai Mohammed Said na (kulia kwa Rais) Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi.(Picha na Ikulu)

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Waumini wa Dini ya Kiislamu kuitikia dua ikisomwa na Sheikh.Shaban Salum Batashi, kumuombea Marehemu Hassan Mohammed Said, baada ya kumalizika kwa Sala ya Maiti iliyofanyika katika Masjid Jamiu Zinjibar Mazizini Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 31-8-2023, na (kushoto kwa Rais) Ndugu wa Marehemu Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mhe. Simai Mohammed Said na Rais Mstaafu wa Zanzibar Alhajj Dkt.Amani Abeid Karume na (kulia kwa Rais) Katibu wa Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Khalid Ali Mfaume na Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Khamis Ramadhan Abdalla.(Picha na Ikulu)


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo Mhe. Zitto Zuberi Kabwe, baada ya kumalizika kwa Dua na Sala ya Maiti ya Marehemu Hassan Mohammed Said iliyosaliwa katika Masjid Jamiu Zinjibar Mazizini Wilaya ya Magharibi “B”Unguja leo 31-8-2023.(Picha na Ikulu)

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Rais Mstafu wa Zanzibar Alhajj Dkt.Amani Abeid Karume,baada ya kumalizika kwa Dua na Sala ya Maiti, kumuombea Marehemu Hassan Mohammed Said, iliyosaliwa katika Masjid Jamiu Zinjibar Mazizini Wilaya ya Magharibi “B”Unguja leo 31-8-2023.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akimfariji na kutoa mkono wa pole kwa Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mhe.Simai Mohammed Said, kwa kufiwa na Kaka yake Marehemu Hassan Mohammed Said, baada ya kumalizika kwa Dua na Sala ya Maiti iliyosaliwa katika Masjid Jamiu Zinjibar Mazizini Wilaya ya Magharibi “B”Unguja leo 31-8-2023.(Picha na Ikulu)

Post a Comment

0 Comments