Ticker

6/recent/ticker-posts

OFISI YA MAKAMU WA RAIS, WADAU WAANDAA TAARIFA YA MKATABA WA MABADILIKO YA TABIANCHI

Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Sigsbert Kavishe akifungua Kikao cha kwanza cha Kamati Tendaji ya Mradi wa Kitaifa wa Kuandaa Taarifa ya Utekelezaji wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi kwa niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga ambapo ametoa wito kwa Wizara za kisekta kutoa ushirikiano katika uandaaji wa taarifa hiyo, kikao kilichofanyika leo tarehe 15 Agosti, 2023 jijini Dodoma.
Wajumbe kutoka Wizara na Taasisi za Serikali wakiwa katika Kikao cha kwanza cha Kamati Tendaji ya Mradi wa Kitaifa wa Kuandaa Taarifa ya Utekelezaji wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi kilichofanyika leo tarehe 15 Agosti, 2023 jijini Dodoma.

Wajumbe kutoka Wizara na Taasisi za Serikali wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa Kikao cha kwanza cha Kamati Tendaji ya Mradi wa Kitaifa wa Kuandaa Taarifa ya Utekelezaji wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi kilichofanyika leo tarehe 15 Agosti, 2023 jijini Dodoma.


Post a Comment

0 Comments