Ticker

6/recent/ticker-posts

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA KONGAMANO LA VIJANA DODOMA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya vijana mara baada ya kufungua Kongamano la Vijana linalofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete mkoani Dodoma. Wengine katika picha kutoka kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Bara Anamringi Macha, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule, Naibu Waziri Tamisemi Deogratius Ndejembi, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Patrobas Katambi, Mbunge wa Kilosa na mtoa mada wa Kongamano hilo Prof. Palamagamba Kabudi pamoja na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Ally Gugu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akihutubia viongozi, watoa mada pamoja na vijana mbalimbali wakati akifungua Kongamano la Vijana linalofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete mkoani Dodoma. Tarehe 07 Agosti 2023.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwasikiliza vijana waliojiajiri kupitia tehama wa Dodoma Data Tech walionufaika na mkopo wa asilimia 4 kwa vijana kupitia Halmashauri wakati akitembelea mabanda ya mbalimbali alipowasili kufungua Kongamano la Vijana linalofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete mkoani Dodoma. Tarehe 07 Agosti 2023.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwasikiliza vijana wanaoshiriki katika Programu ya Kilimo ya Jenga Kesho Iliobora (BBT) Kituo cha Bihawana mkoani Dodoma wakati akitembelea mabanda ya mbalimbali alipowasili kufungua Kongamano la Vijana linalofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete mkoani Dodoma. Tarehe 07 Agosti 2023.

Post a Comment

0 Comments