Ticker

6/recent/ticker-posts

PINDA: HUDUMA ZA AFYA KIBINGWA ZIPELEKWE KILA KANDA


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Dkt. Doroth Gwajima akizungumza kuhusu umuhimu wa kusogeza huduma za matibabu ya kibingwa kwa wananchi alipotembelea banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kuona huduma za upimaji na matibabu ya moyo zilizokuwa zinazotolewa na wataalamu wa taasisi hiyo katika tamasha la Karibu Dodoma festival lililofanyika katika viwanja vya Chinangali park. Kushoto ni Mkurugenzi wa JKCI Prof. Mohamed Janabi.

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Kavuu Mhe.Geophrey Pinda akizungumza na daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Naiz Majani wakati alipotembelea banda la taasisi hiyo kwa ajili ya kuona huduma za upimaji na matibabu ya moyo zilizokuwa zinazotolewa na wataalamu wa taasisi hiyo katika tamasha la Karibu Dodoma festival lililofanyika katika viwanja vya Chinangali park. Katikati ni Mbunge wa viti maalum (CCM) Dkt. Alice Kaijage.


Mkuu wa wilaya ya Dodoma Jabir Shekimweri akimuuliza swali daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Samweli Rweyemamu wakati alipotembelea banda la Taasisi hiyo kwa ajili ya kuona huduma za upimaji na matibabu ya moyo zilizokuwa zinazotolewa kwenye tamasha la Karibu Dodoma festival lililofanyika katika viwanja vya Chinangali park. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa Taasisi hiyo Anna Nkinda.


Mfanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Aliston Jovin akimpatia vipeperushi vinavyoonesha huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo mwananchi aliyefika katika banda la JKCI kwa ajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo zilizokuwa zinazotolewa kwenye tamasha la Karibu Dodoma festival lililofanyika katika viwanja vya Chinangali park jijini Dodoma.


Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Samweli Rweyemamu akimwonesha Mkuu wa wilaya ya Dodoma Jabir Shekimweri mashine ya kiganjani inayopima kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echocardiography) iliyokuwa inayotumika kuwapima wananchi waliohitaji kupata huduma hiyo iliyokuwa inatolewa kwenye tamasha la Karibu Dodoma festival lililofanyika katika viwanja vya Chinangali park.


Fundi sanifu wa moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Gerson Mpondo akimpima kiwango cha sukari mwilini mwananchi aliyetembelea banda la Taasisi hiyo kwa ajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo zilizokuwa zinazotolewa na wataalamu wa JKCI kwenye tamasha la Karibu Dodoma festival lililokuwa linalofanyika katika viwnaja vya Chinangali park jijini Dodoma.

Picha na JKCI

*********************************

Na Mwandishi Maalum – Dodoma

30/10/2021 Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Geophrey Pinda ameiomba wizara ya Afya kusogeza huduma za matibabu ya kibingwa ya kuwafuata wananchi mahali walipo katika ngazi ya mikoa na kanda kwa kufanya hivyo wananchi wengi watafikiwa na huduma hizo.

Pinda ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Kavuu alitoa ombi hilo kwa waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Doroth Gwajima katika tamasha la Karibu Dodoma festival lililofanyika katika viwaja vya Chinangali park ambalo lilikwenda sambamba na zoezi la ushauri, upimaji na matibabu ya magonjwa mbalimbali.

Naibu Waziri huyo ambaye alifika katika banda la Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kupata huduma za upimaji na matibabu ya moyo zinazotolewa na wataalamu wa taasisi hiyo alifurahia huduma zilizokuwa zinatolewa kwa wananchi.

“Ninawapongeza wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete kwa kutoa huduma za matibabu ya moyo kwa wananchi walioko hapa, sijawahi kuona huduma kama hii ikitolewa ninaomba huduma hizi ziende kwa wananchi hadi ngazi ya mikoa na kanda ili watu wengi zaidi wafikiwe na huduma hizi”,.

“Huko vijijini kuna watu wanasumbuliwa na magonjwa mbalimbali yanayohitaji matibabu ya kibingwa lakini wanashindwa mahali pa kupata huduma hizi, kama watu hawa watafikiwa itawasaidia sana kufanya vipimo na kupata matibabu kwa wakati”, alisema Pinda.

Kwa upande wake Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Doroth Gwajima alisema amepokea ombi hilo, atakaa na watalamu wake ili waone ni jinsi gani huduma hizo zinaweza kutolewa kwa wananchi kila baada ya miezi mitatu katika kanda mbalimbali.

“Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amenunua magari yenye x-ray na maabara za kisasa pia wataalamu wako wa kutosha hivyo basi ni rahisi huduma hizi kuwafikia wananchi mahali popote pale walipo”,.

“Ili wataalamu waweze kufika huko wanahitaji kuwezeshwa hivyo basi ni muhimu wapenda maendeleo wakaanzisha kapu la pamoja ambalo litatusaidia kwenda kutoa huduma katika Kanda kwani faida ni kubwa ikiwa ni pamoja na wananchi kugundua matatizo mapema na kupunguza msongamano katika Hospitali za Taifa”, alisema Dkt. Gwajima.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi alisema Taasisi hiyo imekuwa ikitoa huduma za kuwafuata wananchi mara kwa mara na imewasaidia kuwafikia wananchi wengi zaidi ambao wamepata huduma za matibabu kwa wakati.

“Kuwepo kwa huduma hii kumetufanya tufahamu kuwa wananchi wengi wanamatatizo ya moyo hasa shinikizo la juu la damu na hawafahamu kuwa na matatizo haya ndiyo maana kila tunapokwenda kutoa huduma zetu tunaambatana na wenzetu wa kampuni za dawa ambao wanatusaidia kutoa dawa bila malipo kwa wale wote wanaokutwa na shida”, alisema Prof. Janabi.

Post a Comment

0 Comments